UHAKIKI WA MALENGA WAPYA
UHAKIKI WA MASHAIRI YA MALENGA WAPYA MWANDISHI: TAASISI YA KISWAHILI, ZANZIBAR WACHAPISHAJI: OXFORD UNIVERSITY PRESS MWAKA: 2001 JINA LA KITABU Jina la kitabu linasadifu yaliyomo katika kitabu. Kwa upande wa maudhui mambo yanayoelezwa mengi yanaigusa jamii ya sasa. Masuala ya maadili, siasa, uchumi, ukombozi wa kiutamaduni changamoto na suluhisho ya matatizo yanayoikumba jamii yanaendana na wakati wa sasa. Hivyo upya wa malenga wapya ni kweli. Kifani pia Malenga wapya wameweka muundo na mtindo wa kisasa. Malenga wapya ni kitabu kichaozungumzia masuala mbalimbali ya kijami kama vile ukombozi wa mwanamke, umuhimu wa kilimo, umhumimu wa kuondoa matatizo katika jamii, ukombozi wa mwanamke, umuhimu wa kilimo na kadhalika. Ø FANI Fani ni umbo la nje ya kazi za fasihi.Katika ushairi vipengele vya fani vinavyochunguzwa ni:- A. MUUNDO: Hii ni sura, msuko,umbo au uwiano wa vipengele vyote vinavyojenga ushairi. Kuna vipengele kadhaa vinavyotumika kama sehemu ya muundo navyo ni; v