Machapisho

NADHARIA ZA UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI

Nadharia za uhakiki wa kazi za kifasihi 1. Nadharia ya UFEMINISTI   Neno hili linataja jumla ya harakati na itikadi tofautitofauti zinazolenga kufikia usawa wa haki za wanawake katika siasa, uchumi, utamaduni na jamii kote duniani. Wafuasi wa nadharia hii wanashikilia kwamba, pana haja ya kuwa na usawa wa kijinsia licha ya kuwapo kwa tofauti za kimaumbile Hii ni nadharia ambayo haina muhasisi mmoja wala haina msingi mmoja. wanafeministi hutambulishwa kwa wakati na mahali anapotokea.nadharia hii imepata nguvu mwaka 1995. Nadharia hii hudhamiria kuonyesha kwamba uana na uhusiano kati ya mwanaumena mwanamke ni mambo ya kati kabisa katika fasihi. Wahakiki wanaotumia nadharia hii hujikita zaidi katika kutazama jinsi mwanaume alivyo umbwa katika kazi ya kifasihi na kuacha kuitazama kazi inavyosawili maisha yanayo mzunguka mwanadamu. Nadharia hii ya ufeministi imejikita katika msingi mkuu ambao ni kumkomboa mwanamke dhidi ya kani za maisha zinazomdunisha mwanamke katika nyuga zote za mais

UHAKIKI WA MALENGA WAPYA

UHAKIKI WA MASHAIRI YA MALENGA WAPYA MWANDISHI: TAASISI YA KISWAHILI, ZANZIBAR WACHAPISHAJI: OXFORD UNIVERSITY PRESS MWAKA: 2001 JINA LA KITABU Jina la kitabu linasadifu yaliyomo katika kitabu. Kwa upande wa maudhui mambo yanayoelezwa mengi yanaigusa jamii ya sasa. Masuala ya maadili, siasa, uchumi, ukombozi wa kiutamaduni changamoto na suluhisho ya matatizo yanayoikumba jamii yanaendana na wakati wa sasa. Hivyo upya wa malenga wapya ni kweli. Kifani pia Malenga wapya wameweka muundo na mtindo wa kisasa. Malenga wapya ni kitabu kichaozungumzia masuala mbalimbali ya kijami kama vile ukombozi wa mwanamke, umuhimu wa kilimo, umhumimu wa kuondoa matatizo katika jamii, ukombozi wa mwanamke, umuhimu wa kilimo na kadhalika. Ø FANI Fani ni umbo la nje ya kazi za fasihi.Katika ushairi vipengele vya fani vinavyochunguzwa ni:- A.  MUUNDO: Hii ni sura, msuko,umbo au uwiano wa vipengele vyote vinavyojenga ushairi. Kuna vipengele kadhaa vinavyotumika kama sehemu ya muundo navyo ni; v

UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI ANDISHI

Uhakiki wa Ushairi, Tamthiliya na Riwaya Dhana ya Uhakiki Fafanua vipengele vya uhakiki Uhakiki ni kitendo cha kutathmini, kueleza, kuainisha na kutoa maoni juu ya kazi fulani ya fasihi kwa kuongozwa na kaida maalum. Kwa kiwango cha elimu ya sekondari mhakiki anafanya kazi ya uhakiki ili kuonesha mambo yanayojitokeza kama vile, dhamira, migogoro, ujumbe, falsafa, mtazamo, msimamo n.k Dhima ya Mhakiki na Nafasi ya Mhakiki Uhakiki ni kazi ambayo ina mchango mkubwa sana katika kazi za fasihi. Kwa msingi huo uhakiki una dhima zifuatazo: -Husaidia wasomaji kuilewa kazi ya fasihi kwa urahisi;Watunzi wa kazi za fasihi hutofautiana katika matumizi ya lugha na taswira, hivyo mhakiki anapofanya kazi ya uhakiki anamsaidia msomaji kuelewa vipengele hivi kwa kuvifafanua kwa lugha rahisi. -Husaidia ukuaji wa kazi za fasihi;Mhakiki anapoonesha ubora na udhaifu wa kazi ya mtunzi fulani, watunzi wengine pia watafunguka kifikra na kutunga kazi iliyobora zaidi. -Uhakiki hukuza uelewa

UHAKIKI WA MASHAIRI YA CHEKECHEKA

Mwandishi ; Theobard Mvungi Wachapishaji ; EP & D.LTD Mwaka : 1995 Maudhui Dhamira 1. Kutetea Haki Mshairi anamshauri kiongozi wa nchi aendelee kuwasha moto dhidi ya watu wote wanaodhulumu haki za wengine. Katika shairi la MWINYI UMEWASHA MOTO ANGALIA USIZIMWE, mshairi anasema, “Tumaini la wanyonge, kwamba ipo serikali, Ile nchi ya mazonge, ya wenye meno makali, Wanyang'anyao matonge, wanyonge hawana hali, Mwinyi ukiwa mkali, ndio raha ya raia.” 2. Demokrasia Mshairi anapinga mfumo wa chama kimoja. Kwake yeye, mfumo huu, unawanyima watu uhuru wa kutoa maoni yao na kukosoa pale mapungufu yanapojitokea. Shairi hili liitwalo TAIFA WAMELIZIKA liliandikwa kipindi ambacho Tanzania ilikuwa katika mfumo wa chama kimoja. Hata hivyo bado lina uhalisia hasa ukizingatia uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyama vya upinzani leo hii. Mshairi anasema, “Mezikwa demokrasi, Chama kimoja ndo' ngao Watu hawana nafasi, kutetea nchi yao Mawazo ya ukakasi, mawaz